Thursday, February 3, 2011

MAGONJWA YA NGONO

 Napenda kuchukua nafasi hii kuwataka radhi wapendwa wafuatiliaji wa blog hii kwa ukimya uliojitokeza kati kati ya Mwezi Desemba na january mwaka huu, hiyo yote ni kutokana na majukumu ya kujenga Taifa yaliyonibana kwa kipindi hicho.

Ikiwa ni siku ya 34 toka mwaka huu wa 2011 uannze ninayofuraha kubwa kuwajulisheni kuwa mwaka huu hautakuwa kama mwaka uliyopita kwani mtapata vitu adimu na vitamu kwa wakati muafaka.

Nimerejea uwanjani na Gunia zima la utirio hivyo mkae mkao wa kula.

Baada ya kuwadokeza hayo, sasa tuingie moja kwa moja katika mada yetu hapo juu, kwa kifupi tu ni kwamba ili mtu awe na uzazi salama anapaswa kujua yale mambo yanayoweza kuathiri mfumo wake wa uzazi ili kuweza kujiepusha nayo.

Mfumo wa uzazi unaweza kuathiria na mambo mbali mbali ikiwa ni pamoja na magonjwa ya ngono ambayo hushambulia mfumo huo, leo tutajadili baadhi ya magonjwa hayo ambapo tutapata kujua majina yao, jinsi yanavyoambukizwa, dalili na kinga au tiba zao ijapokuwa kipengele cha tiba sitakiongelea kwa undani.

1. KISONONO:
Ugonjwa huu huambukizwa kwa njia ya kujamiiana na mtu mwenye maambukizi na hushambulia zaidi sehemu za siri za jinsia zote.

Dalili;
Dalili kuu za ugonjwa huu ni mgonjwa kutokwa na usaa kwenye sehemu za siri na mgonjwa kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia haja ndogo, na ukikaa kwa muda mrefu bila kutibiwa huenea zaidi kwenye viungo vingine vya uzazi.

Kuzuia/Tiba;
Kinga ya ugonjwa huu ni kuacha kujamiiana au kutumia kondom kwa kila tendo la ngono.
na kwa wale ambao tayari wanamaambukizi wanashauriwa kutibiwa wote hospitalini na kuacha kufanya ngono hadi wapone.


2. KASWENDE:
Huu ni ugonjwa wa ngono unaosababishwa na bakteria.

Dalili;
Mgonjwa wa Kaswende hupata mwasho mkali sehemu za siri na kupata vijeraha vidogo vidogo sehemu hizo na akikaa sana na ugonjwa huo bila kutibiwa huweza kuathirika sehemu zingine za mwili kama vile, Moyo, ubongo na hatimaye kusababisha kifo.

Kinga/ Tiba;
Kinga ya ugonjwa huu ni; kuacha kujamiiana na ukishindwa kuacha kabisa basi fanya ngono iliyo salama(yaani utumie Condom)

Ugonjwa huu hutibiwa Hospitalini na inashauriwa  wenza wenye ugonjwa huu watibiwe kwa pamoja.
Wakati wa matibabu maswala ya kujamiiana yawekwe kando hadi matibabu yakamilike kwani yanaweza yakaongeza maambukizi mapya.

3. KLAMEDIA:
Huu ni mojawapo ya magonjwa ya ngono ambao haujafahamika unaambukizwa na wadudu wa aina gani.

Dalili;
Mgonjwa wa klamedia hutokwa na uchafu  katika sehemu zake za siri na kupata maumivu makali wakati wa haja ndogo na wakati wa kujamiiana.

Kinga/Tiba;
Kinga ya ugonjwa huu ni sawa na kinga ya magonjwa mengine ya zinaa, ili usiupate ugonjwa huu unashauriwa kuacha kabisa kufanya ngono au kutumia condom kwa kila tendo la ndoa.

Hugonjwa huu pia hutibiwa hospitalini.

4. TRIKOMONA:
Ugonjwa huu husababishwa na protozoa (trikomonasi vaginalis) ambazo huambukizwa kwa njia ya kujamiiana.

Dalili;
Dalili za ugonjwa huu hutofautiana kwa kila jinsia.
WANAWAKE: Wanawake wenye ugonjwa huu hupatwa mwasho mkali  katika sehemu za siri,
                           Hutokwa na uchafu wa rangi ya njano au kijani wenye harufu mbaya sehemu za siri.

WANAUME:    Wanaume wenye ugonjwa huu hupata maumivu makali wakati wa haja ndogo.

Kinga/ Tiba;
Ugonjwa huu pia unazuilika kwa kuacha kujamiiana au kutumia condom kwa kila tendo la ngono.
Mgonjwa atatibiwa hospitalini na kupona kabisa.


5.UKIMWI:

Wednesday, February 2, 2011

VYAKULA MUHIMU KWA WAJAWAZITO

kumbuka kwamba vyakula vyote vinaweza kuwa ni muhimu mwilini lakini huzidiana kulingana na mahitaji na hali ya mtu kwa wakati maalumu.

Mahitaji ya madini na vitamini mwilini wakati wa ujauzito huwa ni makubwa, hususani madini ya kashiamu, chuma na Vitamin B9 (folic acid).

MADINI YA KALISI (Calcium)
Wakati wa ujauzito, madini mengi ya kalisi husafirishwa kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kwa ajili ya kuimarisha mifupa na meno. Katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo, mama huhifadhi madini hayo mwilini mwake. Kiumbe kinapokamilisha umbo lake katika kipindi cha miezi mitatu ya mwisho, hifadhi hiyo huanza kutumiwa na kiumbe hicho, hivyo mahitaji yake kuongezeka.

Katika kipindi hiki, mjamzito anatakiwa kula kwa wingi vyakula vinavyoongeza madini ya kalisi kama vile maziwa na vyakula vitokanavyo na maziwa. Kukiwa na upungufu wa madini hayo, meno ya mama na mifupa huathirika pia.

MADINI YA CHUMA (Iron)
Mahitaji ya madini ya chuma nayo huwa makubwa kwa wajawazito. Madini hayo ni muhimu kwa utengenezaji wa damu ambayo huhitajika kwa wingi na mama pamoja na mtoto.

Madini joto hupatikana kwa kula kwa wingi vyakula kama vile nyama, samaki, mayai, vyakula vilivyopikwa kwa nafaka zisizokobolewa (ugali wa dona, mkate mweusi, n.k) na mboga za majani kama vile spinachi na brokoli. Ili kupata madini hayo ya kutosha kutokana na vyakula hivyo, inashauriwa mjamzito kutumia pia vidonge vya Vitamin C (Vitamin C food supplements).

VITAMIN B9 (Folic Acid)
Vitamini hii ni muhimu sana kwa mjamzito, ni kosa kubwa sana la kiafya kwa mjamzito kuwa na upungufu wa vitamin hii. Vitamin B9 ndiyo inayohusika na ukuzaji na uimarishaji wa mfumo wa fahamu wa kiumbe tumboni.

Aidha, Vitamin hii ndiyo inayotoa kinga ili viungo vya mtoto visiathirike na kuepusha uzaaji wa watoto walemavu au wenye kasoro za viungo kama ‘midomo ya sungura’ na kadhalika.

Vyakula vyenye kiwango kikubwa cha Vitamin B9 ni pamoja na mboga za majani, juisi ya machungwa, mapeasi, vyakula vilivyopikwa kwa ngano na mchele (hasa brown rice) na mayai.

Hata hivyo, kutokana na hali ya vyakula vyetu, mjamzito hawezi kupata kiwango kinachotakiwa cha vitamin hiyo kwa kula vyakula peke yake.

Ili kupata kiwango cha vitamin hiyo kinachotakiwa, mjamzito atatakiwa kutumia pamoja na vidonge vya lishe vya Vitamin B9 ili kuepuka upungufu huo. Inashauriwa kutumia vidonge hivyo miezi michache kabla ya kushika mimba na katika kipindi cha miezi mitatu ya mwisho ya ujauzito, kipindi ambacho vitamin hiyo huhitajika kwa wingi.

Kwa ujumla, lishe bora ni muhimu kwa mjamzito katika kipindi chote cha ujauzito wake. Matatizo mengi ya kuzaa watoto wenye ulemavu wa aina mbalimbali, hutokana na upungufu wa madini na vitamin muhimu mwilini katika kipindi cha ujauzito.
 
 
by Gpl.